Sunday, June 1, 2008

chauro





Chauro ni kitafunwa chenye asili ya bara asia kutokana na umaarufu wake wa kulima mpunga pia watu wa bara hilo wamekuwa wabunifu wa mapishi mbalimbali yatokanayo na zao hilo.


Mahitaji


Pepeta ¼
Karanga ¼
Viazi ulaya ¼
Dengu ¼
Chumvi kijiko cha chakula
Sukari kijiko cha chakula
Pilipili ya unga kijiko cha chakula
Mafuta ya kula lita moja

Namna ya kutengeneza

Menya viazi vioshe na vikatekate slesi na kisha weka karai la mafuta jikoni baada ya kuchemka weka viazi na vikaange hadi viive na kukauka, osha karanga na kisha zikaange hadi zikauke osha dengu nazo zikaange baada ya hapo ukivitoa kwenye mafuta vichuje na kisha ziweke hadi zipoe.

Vikishapoa vichanganye na uviweke kwenye chombo chenye nafasi na kikavu halafu nyunyizia sukari kiasi chumvi na pilipili.

Chauro zako tayari kwa kuliwa.

No comments:

Post a Comment