Sunday, June 1, 2008

wali wa kichina

mahitaji

Mchele 1 na 1/2 kilo
Kamba wadogo 1kilo (unaweza kutumia kuku aliyechambuliwa au chaza)
Limau/ndimu 1
Carrot 2-3 (osha kata kwa urefu mara 4 ikisha kata slesi)
Njegere 1/2 kilo
Pilipili boga 1(iliyokatwa vipande vidogo)
Yai 1
Viungo kiasi (pilipili manga, uzile, mdalasini, iliki vilivyosagwa)
Vitunguu maji kiasi (kata vya kukaanga na kutwangwa na thomu)
Thomu kiasi (punje 1-2)
Bizari njano kiasi
Mbatata 2-3 (kata ndogo ndogo ukipenda tia)
Maji kiasi
Mayonaise kiasi(ukipenda)
Mafuta kiasi
Chumvi kiasi

Namna ya kupika

Chemsha kitoweo, chumvi, bizari na ndimu hadi kiwive na kiwe kikavu (au na urojo kidogo), chemsha njegere mpaka zisiwive zikawa laini
Twanga thomu, chumvi kidogo, vitunguu maji na viungo vyote
Chemsha wali kwenye maji ya chumvi na uchuje ukiwa una kiini cha kiasi ya kuwiva, weka pembeni
Weka sufuria unayohisi inaweza kuingia vitu vyote, na utie mafuta
Kaanga vitunguu maji kidogo, mbatata, pilipili mboga, carrot na pia vitunguu vilivyotangwa
Unakoroga kwa muda mdogo hadi zionyeshe kuiva, unatia yai na urojo wa kitoweo kidogo (au mayonaise), ikiasha unamimina kitoweo na njegere
Mwisho unamimina wali na unakoroga hadi uchanganyike na halafu unaonja chumvi kwa kulea ikisha unaoka kwa mkaa kiasi ukauke
Baadae unapakua na unaserve kwa saladi

No comments:

Post a Comment