Friday, September 4, 2009

Kitafunwa cha leo


Mabawa ya kuku/chicken wings

Tukiwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, si vibaya tukaelekezana vyakula vidovidogo vinavyoweza kuliwa mara baada ya futari hususani kwa ajili ya kuchangamsha mdomo.
Leo nimekuandalia mabawa ya kuku au vipapatio kama wengi wanavyopenda kuviita

Mahitaji

Mabawa ya kuku 1/2 kg pilipili manga1/2 kijiko cha mezani chumvi 1 cha mezani
Kitunguu saumu cha kusaga kijiko kimoja 1 sosi ya soya kijiko 1 cha mezani.juisi ya limao vijiko 2 unga wa ngano vijiko 2 vya mezani.
Sosi kali ya ‘periperi’chumvi kijiko 1 cha mezanikitunguu saumu kijiko 1 cha mezanimafuta ya kula ½ kikombe.½ vinegajuisi ya limao vijiko viwili unga wa pilipili nyekundu vijiko viwili.pilipili nzima za kuiva 4-5 pilipili za kashmiri 6
Namna ya kutengeneza

Weka pilipili za Kashmiri, pilipili nzima za kuiva na unga wa pilipili kwenye kikombe cha maji kwa usiku mmoja.
Baada ya hapo saga kwenye blenda kwa muda wa dakika tano.
Weka kwenye bakuli lenye mfuniko na kisha hifadhi kwenye jokofu.

Chukua mabawa ya kuku na yaoshe vizuri kisha yaweke kwenye chombo au bakuli lenye nafasi,
Weka viungo vyote halafu viache kwa muda wa masaa mawili hadi matatu.
Baada ya hapo weka karai la mafuta jikoni tayari subiri hadi yapate moto
Weka jikoni na kaanga hadi viwe na rangi ya hudurungi.

Chakula chako tayari kwa kuliwa andaa chakula hicho pamoja na sosi yako ya periperi ili uweze kupata ladha halisi.

No comments:

Post a Comment