Thursday, August 26, 2010

Juisi ya Bungo


Mahitaji

Bungo 4
Maji 2 Lita (Yaliyochemshwa na kupowa au maji ya chupa)
Sukari 1.5-2 vikombe
Arki (strawberry) kidogo

Namna ya kutengeneza
1) Kata mabungo na yaroweke kwenye nusu lita ya maji au tia ndani ya blender (kokwa za bungo pamoja na maji hadi kwenye alama ya 1lt.
2) Kamua kwa vidole au saga kwa dakika moja tuu (ukiwa hutumii mashine unatumia vidole au mikono tafadhali osha mikono yako kwa sabuni na maji yauvugu uvugu)
3) Kamua mpaka uhakikishe kuwa kokwa hazitoi tena rangi ( kwa ufupi maji mara tatu kwa kutia kwenye blenda na mara nne kwa kutumia mikono)
4) Bakisha nusu lita ya maji kwa kuipika sukari na uchanganye kwenye juice au tia juice na sukari kwenye blender na ukoroge. Ikiwa unapendelea kunywa ikiwa ya baridi si vibaya ukaiweka kwenye jokofu
Mpaka hapo juisi yako itakuwa tayari kwa kunywea.

No comments:

Post a Comment