Saturday, August 21, 2010

Unataka kupungua? fanya haya!

Unene kupita kiasi mara nyingi umekuwa ukichangia kwa kiasi kikubwa kupoteza muonekano mzuri kwa watu wote.
Kwa kufahamu hilo, leo nimeona si vibaya nikakupa ushauri juu ya namna gani ufanye ili kupunguza uzito na umbo lako kwa ujumla.

1. Usiwe mtumwa wa tabia zako!
Kila mmoja wetu na kijitabia chake kilichojificha. Inawezekana wewe una mazoea ya kula sa choklet na soda mara kwa mara. Unaonaje ukibadilika na kutumia vinywaji vya afya kama vile juice za matunda na maji?.

2. Tembea
Kwa kuwa inafahamika fika kuwa kutokana na majukumu ya kikazi tumekuwa tukikosa muda wa kufanya mazoezi. Unaonaje ukatumia muda wako hususani wakati wa kurudi nyumbani. Tembea kadri ya uwezo wako kwani wakati mwingine husaidia kupunguza uzito wa mwili wako.

3. Angalia mlo wako

Kwa kupunguza kiasi cha chakula unachokula katika mlo wako wa kila siku, utaishi maisha ya raha siku zote. Pia utakuwa ukupungua taratibu.


4. Kula chips zenye mafuta kidogo
Ndio, unaweza kufurahia chips zako kuwa kutengeneza zile zinazotumia mafuta madogo. Badala ya kuaanga chukua viazi vyako na vikatekate silesi pulizia mafuta na kisha oka kwenye oven. Tayari utakuwa umepata chips zisizkuwa na mafuta.

5.Usipunguze milo yako
Kamwe usithubutu kuacha kula milo yako ya kawaida. Kula milo mitatu mikuu na mingine miwili ya nyongeza. Lakini ni muhimu kupunguza mlo wako.
6. Jipe kiu
Weka mazoea ya kunywa maji kila mara. Hata pale unaposikia njaa.

7.Usisahau matunda na mboga za majani

Ni vitu ambavyo vitakufanya ujisikie umeshiba muda wote. Na hivyo kukuacha ukiwa mwenye afya njema.

No comments:

Post a Comment